Hamasisiho la Afrika Kwa Ajili ya Usawa katika Kukabiliana na UVIKO-19

Wito wa Kuomba Ruzuku

Tarehe 11 Julai 2022 – 31 Oktoba 2023

Tazama ukurasa huu kwa Kiingereza, Kifaransa au Kiarabu.

Shirika la African Alliance

Dhamira ya Shirika la African Alliance ni kuwa na ulimwengu ambao watu wanaokosa haki na wahanga wa matumizi mabaya ya madaraka wanaweza kuhakikishiwa kwamba kuna watu watakaosimama nao katika juhudi za kujenga jamii inayojali usawa na haki duniani na yenye kuonesha upendo mkubwa katika kutetea, kuhifadhi, kulinda sambamba na kutanua wigo wa haki zao na za watu wengine. Tumekusudia kuendeleza miradi nyeti inayohamasisha, na kuendeleza haki katika kukabiliana mahitaji ya jamii zilizotelekezwa kote barani Afrika kwa kushirikiana katika kuhakikisha kwamba wanajamii wanaonyanyaswa wanaelimishwa kuhusu haki zao, wanapata huduma za afya ya dharura zenye kulinda utu wao sambamba na kuwawajibisha watendaji pale ambapo haki hizi hazipatikani.

Muungano wa Chanjo ya Watu

Muungano wa Chanjo ya Watu ni muungano wa mashirika na mitandao zaidi ya 90, inayosaidiwa na Washindi wa Tuzo ya Nobel, wataalam wa afya, wachumi, Wakuu wa Nchi, viongozi wa kidini na wanaharakati, wanaoshirikiana katika kufanikisha kampeni ya Chanjo ya Watu, inayotolewa kwa kila mtu bila gharama yoyote, sehemu yoyote ile.

Muungano wa Chanjo ya Watu – Afrika

Katika kutambua umuhimu huu – hali ambayo imedhirika kupitia janga hili – tumedhamiria kutafuta suluhu za ndani katika mifumo inayokabiliana na janga hili, kuhakikisha kwamba sauti za Waafrika zinasikika na vipaumbele vyetu vinawekewa msisitizo na kuongeza hamasa, shirika la African Alliance limekuwa jukwaa muhimu ambalo programu ya Muungano wa Chanjo Barani Afrika inatekelezwa. Muungano huu unaosimamiwa kutoka kanda zote tano za bara hili ambapo uenyekiti wake unashikiliwa ni shirika la African Alliance, kazi hii kubwa inayofanywa na Muungano wa Chanjo ya Watu inatumia suluhu kutoka ndani ya Afrika, na inatekelezwa na viongozi wa kanda mbalimbali sambamba na kusimamiwa na mkakati wa kimataifa wa Muungano wa Chanjo ya Watu.

Wito wa Kutuma Maombi ya Kupata Ruzuku ya Kusaidia Kuhamasisha UVIKO-19

Shirika la African Alliance lina furaha kubwa kualika mashirika ambayo yana sifa zilizotajwa hapa chini kutuma maombi ya kupata ruzuku kama Wanufaika wa Ruzuku.

Sifa za Mwombaji

  1. Liwe ni shirika linaloendeshwa na wazawa – Tafsiri yake ni kwamba shirika lako liwe linaendeshwa na watu ambao ni wazawa au wenyeji wa nchi ambako mnatoa huduma. Lazima shirika lako liwe na ofisi au makao yake makuu barani Afrika
  2. Lisiwe Shirika Lisilo la Kiserakli la Kimataifa
  3. Lazima liwe na litekeleze sera inayopiga marufuku ubaguzi dhidi ya kundi lolote lile, ikiwa ni pamoja na lakini sio to Madada Poa, Waraibu wa Dawa za Kulevya, na jamii za LGBTQIA+, Waathirika wa VVU, watu wenye ulemavu, Wafungwa, Wahamiaji, Vijana, Wasichana na Vijana wa Kike
  4. Liwe na washirika au linalotoa huduma katika jamii za maeneo ya mashambani.i
  5. Wadhibitishe kwamba wana sera isiyovumilia na inayopiga marufuku unyanyasaji wa kimapenzi na unyanyasaji wa wafanyakazi wote, wafanyakazi wa kujitolea na watalam, washirika, wanufaika na jamii kwa ujumla.

Wanaotuma maombi pia wataombwa wawasilishe taarifa ifuatayo:

  1. Kibali cha serikali cha kuonesha kwamba shirika limesajiliwa na serikali kama shirika lisilo la kiserikali – tunatambua kwamba sio mashirika yote yatakidhi kigezo hiki, na ikiwa hali itakuwa hivi, mashirika yataombwa yatoe taarifa fupi kutoa sababu ya hali hii; hii inaweza kusababishwa na sheria kandamizi ambazo ni kikwazo kwenye usajili wa makundi au mashirika ya kuhamasisha yanayotetea maslahi ya makundi fulani muhimu ya watu. Katika muktadha huu, kutokuwepo kwa cheti rasmi cha usajili hakutaathiri maamuzi ya ufadhili.
  2. Taarifa kuhusu uongozi wa shirika linalotuma maombi – Tafsiri yake ni kwamba mashirika yanayotuma maombi lazima yawe na muundo wa uongozi unaosimamia maamuzi ya kazi inayofanywa na kundi/shirika au vuguvugu husika na maamuzi haya yanakiliwe kwenye hati na kutiwa saini. Wakati mwingine kundi hili la watu wanaosimamia shirika huitwa Bodi ya Wakurugenzi/Wasimamizi.
  3. Taarifa za usimamizi wa fedha za shirika – Mashirika yataombwa kutuma kumbukumbu zinazoonesha namna wanavyosimamia fedha za shirika. Taarifa hii inaweza kuwa ni tamko la fedha, pia inaweza kuwa kumbukumbu za jumla ya mapato na matumizi ya fedha za shirika.
  4. Taarifa kuhusu timu ya shirika linalotuma maombi ya kupewa ruzuku – hii ni orodha ya watendaji na majukumu yao katika shirika. Taarifa hii itajumuisha msimamizi wa kazi zote zinazofanywa na shirika, hasibu anayetunza kumbukumbu za fedha, mtendaji anayetekeleza shughuli za shirika, mtendaji anayesimamia fedha za shirika na mtu mwingine yeyote anayeshirikiana na timu yenu katika kufanikisha malengo ya shirika.
  5. Orodha ya michango au ufadhili wa fedha mliopata tangu mwaka 2020.
  6. Ushahidi wa barua kutoka kwa washirika wako inayoainisha kazi mliyofanya ndani ya nchi yako.
  7. Nyenzo au zana zozote unazotumia katika kutathmini mwenendo wa kazi yako. Nyenzo hizi zinaweza kuwa ripoti za kila mwezi au kumbukumbu za mikutano.

Mchakato wa Kuchagua na Vigezo na Tarehe

  1. Uchapishwaji wa Wito: Tarehe 12 Mei 2022
  2. Kikao cha mtandaoni cha Maswali na Majibu: Tarehe 19 Mei 2022
  3. Makataa ya kutuma maombi: Tarehe 30 Mei 2022
  4. Uhakiki wa awali ya Sifa za Mwombaji: Tarehe 31 Mei – 3 Juni 2022
  5. Uorodheshaji wa wanufaika – kwa kuzingatia RFP na mabadiliko wanayoweza kuleta: Tarehe 6 – 10 Juni 2022
  6. Kamati ya Uendeshaji ya PVA itapitia orodha ya waombaji walioorodheshwa: Tarehe 13 – 17 Juni 2022
  7. Kamati ya Uendeshaji ya PVA itapiga kura: Tarehe 20 Juni 2022
  8. Mashirika yote yaliyotuma maombi yatapata majibu ya mchakato huu: Tarehe 21 Juni 2022
  9. Tathmini ya ufaafu wa mashirika yaliyochaguliwa kunufaika na ruzuku itafanyika: Tarehe 22 Juni – Tarehe 1 Julai 2022
  10. Mikataba yote itakamilishwa na awamu ya kwanza ya ruzuku itatumwa kwa waombaji: Tarehe 8 Julai 2022
  11. Tangazo rasmi kuhusu Mashirika Yaliyoshinda Ruzuku: Tarehe 4 Julai 2022
  12. Utekelezwaji wa mradi unaanza rasmi: Tarehe 11 Julai 2022

Ni utaratibu gani tutatumia kuchagua Mshindi wa Ruzuku?

Mchakato wa kuchambua maombi utasimamiwa na Kamati ya Uendeshaji ya PVA, ambayo inaundwa na wawakilishi wa mashirika ya uraia kutoka kila kanda ya Afrika.

Hatua za Mchakato:

  1. Hatua ya kwanza ya mchakato wa kuchagua ni kutathmini kiasi ambacho mwombaji anatosheleza vigezo na mchakato huu unaendeshwa na Sekretarieti ya Afrika ya PVA wakisaidiwa na Kamati ya Uendeshaji ya PVA Afrika. Maombi yote ambayo hayakidhi vigezo vilivyowekwa na hayana maelezo ya kuridhisha kuelezea sababu ambazo zinafanya shirika lisifuate sheria husika, yataingia katika hatua zinazofuata.
  2. Hatua ya pili inahusu mchakato wa uhakiki wa mtandaoni utaratibu utakaofanywa na wawakilishi wa Kitengo cha Fedha na Ruzuku kutoka shirika la African Alliance ili kubaini hatari zozote zinazoweza kukabili shirika la African Alliance. Ikiwa kuna ulazima, basi mashirika yatakayopata ruzuku hii yatapata msaada wa kujengewa uwezo
  3. Hatua ya tatu ya mchakato huu wa uhakiki ni Sekretarieti ya PVA Afrika na Kamati ya Uendeshaji ya PVA Afrika kushauriana zaidi kuhusu matokeo ya hatua za awali za uhakiki kisha wakubaliane orodha ya mashirika yatakayopata ruzuku kwa kuzingatia njia inayopendekezwa na shirika, jinsi inavyoingiliana na kazi na mkakati wa sasa wa PVA, na uwezo wake wa kutekeleza mikakati sawa.

Kipaumbele

  1. Kuhamasisha mikakati inayohimiza upatikanaji wa chanjo, vipimo, na matibabu ya UVIKO-19 kwa usawa, bei nafuu, na kila mahali kitaifa na kikanda
  2. Kampeni za kuelimisha kuhusu mchango wa makampuni ya dawa katika kudhibiti janga la UVIKO-19
  3. Kuhamasisha kampuni za kutengeneza dawa kutoa leseni kwa dawa za sasa zilizoidhinishwa kutumika katika Nchi Zote za Uchumi wa Chini. Hii ni pamoja na mashirika kama vile WTO, WHO, UNITAID, na Wakala wa Dawa Barani Afrika miongoni mwa mashirika mengine.
  4. Kuhamasisha uwazi wa ndani ya nchi katika mipango yote ambayo imefadhiliwa, ikiwa ni pamoja na chanjo ya UVIKO-19, vipimo na matibabu
  5. Kuimarisha ujuzi ikiwa ni pamoja na matangazo ya vyombo vya habari na Haki Miliki
  6. Kuanzisha kampeni za hamasa

Bajeti na Maeneo Ya Kipaumbele Kijiografia

Afrika Kaskazini

Ruzuku 2 za thamani ya ZAR 280 000 kwa kila moja katika kipindi chote cha mradi huu

  • Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria
  • Jamuhuri ya Kiarabu ya Egypt
  • Jamuhuri ya Kiarabu ya Mauritania
  • Ufalme wa Morocco
  • Sahrawi Arab Democratic Republic
  • Jamuhuri ya Tunisia
  • Libya

Afrika ya Kati

Ruzuku 2 za thamani ya ZAR 280 000 kwa kila moja katika kipindi chote cha mradi huu

  • Burundi
  • Cameroon
  • Chad
  • Congo
  • Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo
  • Equatorial Guinea
  • Gabon
  • São Tomé and Principe

Afrika Mashariki

Ruzuku 2 za thamani ya ZAR 280 000 kwa kila moja katika kipindi chote cha mradi huu

  • Comoros
  • Djibouti
  • Eritrea
  • Kenya
  • Madagascar
  • Mauritius
  • Rwanda
  • Seychelles
  • Tanzania
  • Uganda
  • South Sudan
  • Sudan
  • Ethiopia
  • Somalia

Kusini mwa Afrika

Ruzuku 2 za thamani ya ZAR 280 000 kwa kila moja katika kipindi chote cha mradi huu

  • Angola
  • Botswana
  • Kingdom of eSwatini
  • Lesotho
  • Malawi
  • Mozambique
  • Namibia
  • South Africa
  • Zambia
  • Zimbabwe

Afrika Magharibi

Ruzuku 2 za thamani ya ZAR 280 000 kwa kila moja katika kipindi chote cha mradi huu

  • Benin
  • Burkina Faso
  • Cabo Verde
  • Côte d’Ivoire
  • The Gambia
  • Ghana
  • Guinea
  • Guinea-Bissau
  • Liberia
  • Mali
  • Niger
  • Nigeria
  • Senegal
  • Sierra Leone
  • Togo

Kumbuka kwamba miradi hii si lazima itekelezwa katika kipindi chote cha ruzuku hii (Tarehe 1 Julai, 2022 – Tarehe 31 Oktoba31 2023) lakini inaweza kutekelezwa katika ndani ya muda mfupi.

Unaweza kushirikiana na mashirika mengine yanayopatikana katika kanda yako. Lakini unaruhusiwa kushirikiana na shirika moja pekee. Hata hivyo, ni shirika moja pekee (mwombaji mkuu wa ruzuku) ndilo litakalopewa ruzuku na ndilo litakalokuwa na wajibu wa kutuma ripoti za kazi iliyofanywa.

Ikitokea kwamba pendekezo moja kutoka kanda fulani limeshinda, Kamati ya Uendeshaji ina haki ya kutoa ruzuku yote ya kanda kwa mwombaji huyo pekee katika kanda yote.

Ni waombaji ambao maombi yao yataoorodheshwa pekee ndio watakaoalikwa kuendelea na hatua zinazofuata.

Tarehe Muhimu

Siku ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 30 Mei 2022. Tunahimiza kwamba utume maombi mapema kwa sababu hatutapokea maombi kupitia mfumo wa mtandaoni baada ya tarehe ya mwisho na maombi yatakayotumwa kwa njia ya barua pepe hayatakubalika.

Maswali

Kando na kikao cha mtandaoni (Webinar) cha tarege 19 Mei 2022, unaweza kutuma maswali kwa granteesupport@africanalliance.org.za hadi tarehe 26 Mei 2022. Majibu ya maswali haya yatakusanywa na kuchapishwa hapa na tutaendelea kuyajibu kadri tutakavyopokea maswali hadi siku ya mwisho.